Watu wengi wanaona wakati ajali barabarani inapotokea, abiria wanaokaa kando ya dereva wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi, na abiria wanaokaa nyuma ni salama zaidi.
Je, mtazamo huu ni sahihi?
Polisi wa Japan wamechambua idadi ya watu waliofariki kwenye ajali za barabarani na kugundua kuwa mtazamo huo si sahihi.
Mwaka 2016 watu 3,904 walifariki kwenye ajali za barabarani nchini Japan ambapo kati yao watu 1,338 walikuwa abiria; asilimia 0.36 ya abiria waliokaa kwenye viti vya nyuma, asilimia 0.32 ya madereva, na asilimia 0.27 ya abiria waliokaa kando ya madereva walifariki.
Hivyo, watu wanaokaa nyuma wako hatarini zaidi kuliko wale wanaokaa kando ya madereva wakati ajali zinapotokea.
Polisi wa japan wamesema, zamani ilikuwa hatari kukaa kwenye viti vya mbele, lakini teknolojia inayotumika katika magari yanayotengenezwa siku hizi yana mifuko ya hewa na mikanda ya viti hivyo madereva na abiria wanaokaa mbele wanalazimika kufunga mikanda na kupelekea hivyo idadi ya vifo vinavyotokana na ajali za barabarani kupungua kwa kiasi kikubwa.

Lakini abiria wengi wanaokaa nyuma bado hawafungi mikanda, na kuwafanya wawe hatarini wakati ajali zinapotokea.
Kwanini abiria wanaokaa viti vya nyuma hawafungi mikanda? Ni kwa sababu watu wengi huamini kuwa wapo salama zaidi pindi inapotekea ajali ya gari.
Hata nchini Tanzania watu wengi wanaokaa viti vya nyuma hawafungi mkanda kwa dhana kama hiyo. Na pindi inapotokea ajali hutupwa nje ya gari kwa kuwa hawakufunga mkanda.