Wezi watatu wameiba Simu mpya za iPhone X baada ya kuvunja gari maalumu la kubebea mizigo la kampuni ya UPS lililokuwa limehifadhi simu hizo nje ya duka la Apple huko San Francisco nchini Marekani.
Tukio hilo la wizi lilitokea asubuhi ya siku ya Jumatano; inaelezwa watu watu waliokuwa wanaendesha gari nyeupe aina ya Dodge van walipita karibu na gari la UPS lilokuwa linajiandaa kushusha mzigo katika Stonestown Galleria shopping mall huko San Fransisco, ndipo ulipovunjwa mlango na kuondoka na furushi lililokuwa na simu hizo.
Tukio hilo linaloonekana kama la kupangwa wafanyakazi wa Apple na UPS wanaisaidia polisi katika upelelezi wake wa kuwapata wezi hao. Mpaka sasa watu hao wajajulikana wala kukamatwa. Taarifa zinasema simu hizo zilizoibwa zinaweza zisiweze kutumika ndani ya Marekani kwani namba zake za IMEI zimehifadhiwa na ni rahisi kuzifunga.