Amit Fulay aliyekuwa mkuu katika kampuni ya Google kwenye uzalishaji wa Programu za Allo na Duo ameondoka na kujiunga rasmi na Facebook.
Taarifa ya kuondoka Google na kujiunga Facebook, Amit Fulay aliitoa mwenyewe kupitia ukurasa wake wa Twitter Jumanne wiki hii.
Amit ni miongoni mwa watu muhimu waliohusika katika kujenga programu ya Hangout, Allo na Duo. Programu zote hizo ni mawasiliano ya watu kwa njia ya ujumbe wa maneno, sauti pamoja na picha za video.
Bw. Amit fulay amedumu katika Google (kampuni) kwa miaka 7 na miezi 5 akiwa sehemu ya watu muhimu waliotoa mchango mkubwa ndani ya kampuni hiyo (Google).