Mwanaume mmoja huko nchini India katika jimbo la Assam afanyiwa upasuaji wa kutolewa chaja ya simu mwilini mwake. Upasuaji huo ulitegemewa kuwa wa kawaida ila ukawa usio wa kawaida.
Mgonjwa huyo, mwanaume wa miaka 30 alienda akidai anasikia maumivu makala eneo la chini la tumbo na hii ni baada ya yeye kumeza chaja ya simu ya urefu wa futi 2. Ila mwisho wa siku ikaja kuonekana alidanganya, chaja hiyo ilikutwa kwenye kibofu cha mkojo.
Ilikuwaje:
Madaktari mwanzo walimpatia dawa za kuharisha wakidhani ataweza kutoa waya huo kupitia haja kubwa. Baada ya kuona haijatoka wakaamua kumfanyia vipimo vya X-ray. Hapo ndipo wakagundua ya kwamba mwanaume huyo alidanganya, waya huo upo kwenye kibofu cha mkojo.
Inasemekana mwanaume huyo ana tabia za ajabu za kingono zinazohusisha kujiingiza vitu kupitia uume wake.
Madaktari walifanikiwa kumfanyia upasuaji na kuutoa waya huo. Kwa sasa anaendelea na matibabu na wanaamini atapona vizuri.
Vyanzo: HindustanTimes