Katika maonyesho makubwa ya kompyuta na vifaa vingine vya kielektroniki yaliyofanyika huko Taiwan, Acer wameibuka na kusema kuwa kuna matoleo kadha ya Tabiti ambayo wanatarajia kuyaweka sokoni
Kumbuka Acer ni mmoja kati ya watengenezaji wazuri sana wa kompyuta. Mimi binafsi walinifurahisha sana walivyokuja na Acer Chrome Book.
Ukitaka kujua zaidi kuhusiana na laptop za Chrome Book Bofya Hapa
Katika maonyesho hayo makubwa yanayojulikana kama computer and consumer technology trade expo, Acer walisema kuwa kutakua na matoleo mawili katika tabiti hizo
Toleo La Kwanza
- Iconia Tab 10
japokuwa hawakuweka wazi taarifa nyingi kuhusiana na tabiti hii lakini ni kwamba itakuja na kioo chenye ubora wa ‘quantum dot’ ambacho kwa haraka haraka kitakua kinang’arisha rangi
Kwa upande wa CPU pia ni kwamba itakua inaendesha na mfumo endeshaji wa Android (Android Nougat) na pia uwezo wake wa sauti utakua ni ule wa HD.
Uwezo wake wa kukaa na chaji ni masaa nane (8). Kwa upande mwigine unaweza ukasema kuwa Tabiti hii haitakua ya kufanyia kazi ngumu moja kwa moja kama vile kucheza gemu na kuitumia katika programu kubwa kubwa. Lakini kwa kazi kama za kuangalia video n.k hapo ndipo pake.
Cha kushangaza ni kwamba Tabiti hii bado inatumia jina linalofanana na tabiti iliyopita katika kampuni hilo hilo. Pengine labda kampuni lina maana yake, kwa upande wangu naona hilo sio jambo jema.
Toleo La Pili
- Iconia One 10
Toleo hili ndilo ambalo limedhamiriwa kuwa litakuwa linahimili kazi nzito nzito ambazo kwa namna moja au nyinigne toleo la juu litashindwa fanya.
Hii na yenyewe itakua na programu endeshaji kutoka Android (Android Nougat) na pia itakuja na sehmu mbili la kuweka USB lakini kingine cha kushangaza ni kwamba katika matundu hayo ni tundu moja tuu ambalo ndio litakuwa na uwezo wa USB OTG (On-The-Go). Kwa hiyo hapa kwa haraka haraka ni kwamba uunganishaji wa vifaa mbalimbali na tabiti hii utakua ni mdogo.
Hitimisho
Kama kampuni haitafanya juu chini na kujitahidi kuongeza baadhi ya vitu au kutupa sifa (specification) zingine ukiachana na hizi ambazo zinajulikana mpaka sasa bado watu watajiuliza sana katika kuzinunua
Kwa sasa duniani kote kuna ushindani mkubwa sana na wateja mara nyingi hawapendi kununua viitu ambavyo viko kawaida katika swala zima la teknolojia.
Lakini vile vile ndio tabia ya Acer tokea mwanzo. Kampuni haijawhii kukaa na kutoa bidhaa ambayo itaishangaza dunia lakini mara nyingi wao hutengeneza bidhaa za kawaida ambazo zinakua zinauzwa kwa bei nafuu kabisa — pengine bado hili ndio lengo lao — kwa wateja wao.
Hapa hatuna sababu ya kuongelea sana Tabiti hizi kwani hatujua sifa nyingi za ndani ambazo hazikuwekwa wazi. Vile vile kampuni haikuweka wazi kuwa tabiti hizi zitaingia rasmi sokoni (tarehe)