Kumbuka tulishawahi andika kuhusu App ya UberEats, App ambao inawawezesha watu kuagiza na kuletewa msosi, kwa sasa kampuni mama yaani Uber imeona ni vyema kabisa kwa App hiyo kuhama na kuingia ndani ya App kuu.
Kuhusu Uber Eats Soma Tena Hapa
Lakini japokua kutakuwa na mabadiliko hayo (UberEats ndani ya Uber) bado App ya UberEats ambayo inajitegemea itakuwepo kama kawaida. Japokuwa katika App mabadailiko ni bado hayajaanza kuonekana katika baadhi ya nchi, lakini katika tovuti ya Uber tayari kuna kipengele cha Uber Eats.
Kampuni imesema imefanya hivi makusudi kabisa katika kuhakikisha kuwa wateja wake wanapata huduma bora kabisa ambayo wataifurahia. Kingine kikubwa ni kamba kampuni ina imani kubwa kuwa kwa kuziweka huduma hizo mbili zote pamoja basi kampuni itaweza kuaongeza matumizi ya kila huduma kutoka kwa wateja.
Kingine ni kwamba kuna baadhi ya sehemu huduma hii inaweza ikawa haijafika kwani ndio kwanza ipo katika hatua za mwanzo na mara nyingi kama inavyojulikana inaweza ikawa ndio wakati wa majaribio.
Mara ya kwanza Uber walikua wanaona kama kuagiza chakula na kuagiza usafiri ni vitu viwili ambavyo haviendani lakini sasa wamebadilisha mawazo yao na kwenda kinyume.
Ikumbuke pia kuwa App ya Uber ni App namba moja duniani katika maswala ya usafiri,hivyo ni wazi kabisa kuwa jambo hili linaweza kwa kiasi kikubwa kuinua zaidi biashara hizo mbili.