Je unazijua simu za Samsung zinazouza kwa sana India? Samsung nchini India imetangaza kwa vyombo vya habari kuwa imeuza simu milioni 2 za Galaxy J6 na Galaxy J8 ambazo zimezinduliwa karibuni.
Kupitia Makamu Rais Asim Warsi wa Samsung India, kampuni hiyo ilidai kuwa aina za simu hizo zilivutiwa wateja wengi hivyo kufikia mauzo ya simu 50,000 kwa siku tangu uzinduzi wa J6 mwezi Mei 22 na J8 mwanzoni mwa mwezi Julai.
Mafanikio hayo yametokana na falsafa yao ni kuweka masikio yao kwa wateja na kutekeleza kile wanachotaka na kupendekeza kukiona kwenye simu zao za Samsung.
Samsung Galaxy J6 ilikuwa simu yenye bei nafuu yenye kioo cha AMOLED,
- prosesa ya Exynos 7870,
- ukubwa wa uhifadhi wa 32GB na RAM ya GB 3
- ikiwa na kamera ya 13MP.
Kwa upande wa Galaxy J8 inakuja na kamera mbili za nyuma 16MP+5MP,
- betri lenye mAh 3,500
- RAM GB 4,
- uhifadhi wa ukubwa wa GB 32 na GB 64
- prosesa ya Snapdragon 450.