Pokemon Go ni moja kati ya magemu katika simu ambayo yamejopatia umaarufu mkubwa sana na pia ni moja kati ya gemu ambalo limeiingizia kampuni ya Niantic mapato mengi.
Ukaichana na umaarufu ambao kampuni imeupata kupitia katika gemu hii badi hailali maana kwa sasa wana mpango wa kuja na mtandao wao wa kijamii
Mtandao huu utakua –tunachojua mpaka sasa — ni mahsusi kwa ajili ya magemu yanayotengenezwa na kampuni hiyo.
Jina la mtandoa huo umepewa jina la Campfire, na uko tayari hivyo basi utaachiwa rasmi siku za usoni.
Kwa sasa kinachoendelea ni kwamba mtandoa upo katika hatua za majaribu ili kuahakikisha kuwa unaenda sambamba na magemu husika .n.k.
Kikubwa ambacho mtandao huu utafanya ni kama kukutnaisha marafiki, kujua marafiki wa karibu, kuhudhuria matukio kadha wa kadha ambayo yameandaliwa na wachezaji.
Kama mitandao mingine ya kijamii tuu, hata katika mtandao huu kutakuwa na huduma za kutuma na kupokea ujumbe (DM)
Bila kusau kuwa mpaka sasa kampuni ya Niantic ina huduma nyingi sana na magemu ya aina mbalimbali hii itasaidia kwa kuhakikisha kuwa inayaweka pamoja ili watu wafurahie.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je utawweza kutumia mtandao huu?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.