Teknolojia kuchukua ajira mbalimbali katika miaka ya hivi karibuni. Utafiti unaonesha nusu ya ajira zote duniani kuchukuliwa na teknolojia kufikia mwaka 2035. Hii ni takribani ajira milioni 800.
Utafiti uliofanywa na kitengo cha utafiti cha Benki ya Marekani (BofA Securities) unaonesha kuna uwezekano teknolojia kuchukua nusu ya ajira zote duniani kote kuchukuliwa na vifaa vya kisasa vya teknolojia kufikia mwaka 2035.
Utafiti huo unaonesha roboti wanazidi kuwa bei nafuu zaidi na wakati huo huo wanakuwa na akili zaidi kulingana na maendeleo ya teknolojia.
Roboti wa viwandani wameshuka bei kwa takribani asilimia 27 ukilinganisha bei ya mwaka 2005 hadi bei ya mwaka 2014. Bei itashuka tena kwa asilimia 22 kufikia mwaka 2025.
Utafiti huo unaona teknolojia na utumiaji wa roboti hautachukua ajira kwenye viwanda tuu, bali ata kwenye sekta za huduma za kibiashara na maofisini. Kuna programu/apps mbalimbali zinazoelekea kuondoa uwepo wa ajira kwa binadamu.
Uwezo wa China kukua kwa kasi katika teknolojia za maroboti zimefanikisha kushuka kwa bei za teknolojia hiyo kwenye soko la dunia. Watafiti wanaamini China imefikia katika hatua kubwa ya kuweza kuwa kiongozi wa teknolojia za kisasa za kompyuta zitakazochukua ajira kufikia mwaka 2030.