Akiwa kama mtengenezaji mkubwa wa vifaa vya elektroniki, kampuni ya Samsung imeendelea kupanua shughuli zake za viwanda ulimwenguni kote.
Samsung wametangaza kufungua milango ya maendeleo katika mji wa Noida nchini India kwa kufungua kiwanda kikubwa cha kutengeneza wa simu. Hata hivyo, wana viwanda nchini za Marekani, Brazil na Korea Kusini kama makao makuu. Kukua kwa ufanisi wa simu za Samsung kupelekea kampuni hiyo kuwekeza kwa kufungua kiwanda katika nchini India.
Kiwanda hicho kinatarajiwa kuzalisha simu milioni 120 kwa mwaka. Mbali na simu pia watakuwa wanatengeneza TV na majokofu. Eneo ambalo kiwanda hicho kitajengwa lina ukubwa wa ekari 35.
Takwimu zinaonyesha asilimia 10 ya simu zinazozalishwa na Samsung zinanunuliwa katika soko la India.
Sababu kubwa ya kuanzisha kiwanda India ni mahitaji wa simu yamekuwa makubwa sana ambapo India ni soko kubwa duniani nyuma ya soko la Uchina.
Katika kiwanda hicho cha Samsung kinatazamiwa kutengrza simu karibu mara mili ya idadi ya sasa mpaka kufikia mwaka 2020 kitu ambacho kitaongeza soko la simu zake mpaka kufikia asilimia 50 kwa India.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.