Inasemekana kuwa simu za Samsung katika mwendelezo wake wa matoleo ya Galaxy wako mbioni kuleta toleo liningine sokoni
Baada ya Samsung Galaxy S8 sasa ni zamu ya S9 — Pia inasemekana kuwa matoleo haya yatatoka mawili yaani S9 na S9 Plus.
Kampuni ipo katika matengenezo ya simu hizo mbili na ili kuhakikishai watu kuwa simu hizo zipo katika matengenezo wameweza pia kuweka wazi namba za modeli ya simu hizo, G960FXXU0AQI5 kwa ajili ya Galaxy S9 na G965FXXU0AQI5 kwa ajlli ya S9 Plus.
Watabiri wengi wamesema simu hiyo itakuja na angalau GB 4 katika ujazo wake wa RAM, Pia itakuja na kamera mbili (dual) kama ilivyokua kwa Note 8.
Itakua inaendeshwa na Android Orea tangia mwanzo kabisa. Kingine ni kwamba inasemekana kuwa Galaxy S9 zitakuwa na umbo sawa sawa kabisa na matoleo ya Galaxy s8. Hii inaonyesha kabisa kuwa kampuni inajikita zaidi katika ubunifu wa nadani ya simu na sio kuongeza ukubwa wa skrini ya vifaa vipya.
Mambo yakikaa sawa, kampuni inaweza ikaitoa simu hiyo mwezi Aprili mwaka 2018. Inaweza ikaonekana kama ni mbali ila kwa siku zinavyokumbia ni kesho tuu hivyo tusubiri….