Je ni mambo gani muhimu ya kuzingatia katika kutengeneza Password a.k.a nywila iliyo salama zaidi? Leo tutakufundisha jinsi ya kufanya hivyo.
Nywila ni neno sanifu la Kiswahili kwa ajili ya neno “Password”. Maneno mengine ambayo hutumika kwa umaarufu zaidi ni kama Nenosiri na Neno la Kificho.
Hii ni moja ya njia za kuweka usalama katika taarifa mbalimbali katika mifumo ya kielektroniki kupitia simu , tarakilishi (kompyuta) ama vifaa vyovyote vya kielektroniki vyenye uwezo wa kufungua taarifa hizo.
Mifumo mbalimbali ya kielektroniki huwa na vigezo ambavyo vimewekwa kwa ajili ya utengenezwaji wa Nywila. Vigezo hivi huwa na uhusiano toka mfumo mmoja hata mwingine maana ni njia ya kuweka ulinzi ambayo ni maarufu na hutumika zaidi. Baadhi ya vigezo hivyo ni.
- Lazima iwe na herufi zisizopungua sita (6), ama nane (8), kutegemeana na mfumo.
- Lazima iwe na mchanganyiko wa herufi (A-Z), tarakimu (0-9), na alama mbalimbali.kama #,+ n.k..
- Kuwa na mchanganyiko wa herufi kubwa na ndogo.
Vigezo hivi ni vya msingi katika kuimarisha usalama wa nywila yako kutambulika na wewe binafsi , hivyo kuifanya kuwa salama na ngumu kwa mtu mwingine kuidukua.
Nia kuu ya Nywila ama Nenosiri ndio faida yake kuu pia. Nayo ni kuweka ulinzi wa taarifa za mtu binafsi, kikundi cha watu, taasisi ama shirika zilizo katika mfumo wa kielektroniki.
Kwa sababu nywila huweza kubeba mchanganyiko wa herufi, tarakimu na alama mbalimbali, hii humaanisha uwanja mpana wa uchaguzi wa nywila ili kutokuwa rahisi kwa mdukuzi.
Pamoja na hayo, kuna hatua mbalimbali za kiusalama za kuchukua ili kuhakikisha usalama binafsi wa nenosiri lako, ikiwemo.
- Kubadilisha nywila ama nenosiri kila baada ya siku 90 (miezi mitatu)
- Kutowashirikisha nywila yako watu wengine kama marafiki na watu wa karibu.
- Kufunga akaunti ama mfumo wenye taarifa zako (logging out) mara baada ya matumizi, hasa ukiwa ulifungua kwenye kifaa kisicho chako.
- Kutokutumia nywila sawa katika mifumo/huduma mbalimbali, maana ni hatari. Endapo itadukuliwa, mifumo yote itakosa usalama
Soma Makala zingine zinazohusu Maujanja ya kwenye Simu na Kompyuta -> Teknokona/Maujanja
No Comment! Be the first one.