Twitter imeongeza kipengele ambacho kinajulikana kama ‘Tweet Scheduling’ ambacho kina maana ya kuwa mtumiaji wa twitter unaweza uka’tweet kitu lakini kitu hicho kikapanda katika ukurasa wake kwa muda wa mbele kabisa ambao utakua umeuchagua yeye.
Ni wazi kuwa hapo zamani kitu hiki kilikua kinashindikana kabisa kwa kutumia akaunti kuu na App ya twitter.. kuwezekana kufanyika kwa hili ilikua ni lazima kutumia App mbadala kama vile TweetDeck.
Ukitaka kuwezesha kufanikisha hili hakikisha katika kompyuta (bila kutumia App) kisha ingia katika mtandao wa Twitter. Katika eneo la kuandika tweet kwa chini utaona kuina kialama cha kalenda. Ukiingia katika kialama hicho utakua na uwezo wa kuandika tweet unayotaka na kuiamuru iruke baadae kulingana na muda ambao wewe utakua umependekeza.
Najua swali ambalo unajiuliza hapo ni kwambi vipi kuhusu katika App zako za simu?. Kiukweli ni kwamba Twitter imekua ikihangaikia katika kufanya kipengele hiki kinawezekana kwa muda mrefu tuu sasa.