Huduma ya Alexa kutoka Amazon haina utofauti mkubwa na huduma ya Siri kutoka Apple.
Ni huduma ya roboti ambayo inarahisisha matumizi ya kifaa cha kielektroniki na wewe ndio unakua una uwezo wa kuamuru nini unataka roboti huyo akufanyie
Kwa sasa Amazon imesema ipo katika hatua za kudumisha kumbukumbu kwa watu hata kama kuna mtu atafariki basi Alexa itaweza kuigizia sauti yake.
Huduma ya Alexa imekua ikipatikana kwa kipindi cha muda mrefu tuu na kwa sasa kuna maboresho ambayo kampuni inayafanya ili kuwezesha hili na hivyo bado kampuni haijaweka wazi kuwa ni lini kipengele hiki kitaanza kutumika rasmi.
Lakini kingine kikubwa ni kwamba teknolojia hii sio lazima itumike katika kudumisha kumbukumbu kwa mtu aliefariki tuu, kuna nama nyingi inaweza kutumika (hata kuiga sauti ya mtu alie hai-sio?)
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, hii umeipokeaje? Je unaweza ukatumia teknolojia hii kama kumbukizi kwa mtu aliekutoka?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.