Kampuni ya Sony inajishushisha na mambo mengi sana yakiwemo na yale ya kiteknolojia. Sony ndio inamiliki vifaa vya michezo vijuilkanavyo kama PlayStation (PS).
PlayStation (PS) zipo kwa matoleo na mpaka sasa wapo katika toleo la tano ps5, na wametoa idadi ya mauzo ya vifaa hivyo.
Kwa robo ya mwaka iliyopita pekee Sony wameweza kuuza idadi ya PlayStation (PS) 5 zipatazo milioni mbili tuu na hii ndio imepelekea mpaka kampuni kufikisha mauzo ya milioni 19.3.
Kwa sasa inasemekana kuwa mauzo ya kampuni hiyo kwa vifaa hivi yanapungua sababu ukifananisha mauzo ya robo ya mwaka huu na robo ya mwaka wa jana kuna tofauti kubwa ya mazidiano.
Kingine ni kwamba kampuni ya Sony imekiri kuliona hili na sababu iko sana sana katika upande wao na sio katika upande wa wateja.
Kinachopelekea uzalishaji kuwa mchache ni sababu zitokanazo na uhaba wa chipu (chip) ambazo zinatumiaka katika kutengeneza PlayStation (PS) 5 hizo.
Wataalam kutoka Sony wameshaliona hilo na wanatabiri kutakua na ongezeko la asimia 34 katika mauzo yake, hapa hatuna budi bali kusubiri tuu.
Ningependa Kusikia Kutoka Kwako, Niandikie Hapo Chini Katika Eneo La Comment Hii Umeipokeaje Kutoka PlayStation (PS) 5?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.