Katika uandishi kwenye mitandao ya kijamii emoji zinachukua nafasi kubwa hasa katika kunogesha mazungumzo, kila mwaka muungano wa Unicode (ambao ndio unaamua emoji gani zitumike) hukaa na kuamua waongeze emoji mpya zipi katika orodha ya emoji.
Mwaka huu muungano huu umekwisha kaa na tayari umetoa mapendekezo ya emoji mpya kwaajiri ya mwaka 2017.
Unicode wamependekeza emoji 51 ambazo bado zilikuwa hazipo katika matoleo yaliyopita, emoji hizi kama zitapita basi zitaanza kutumika mwakani. Ni bado mapema saana kujua kama emoji zilizopendekezwa ndio zitakazopitishwa kuna uwezekano yakafanyika mabadiliko kadhaa.
Kwa watumiaji wa android basi watakaozipata ni wale tu ambao watakuwa wanatumia vifaa ambavyo vitakuwa na OS zilizotoka baada ya toleo hili la emoji lakini kwa wale ambao wanatumi iOS basi wao watazipata emoji hizi baada ya kuanza kutumia toleo jipya la iOS.
Katika pendekezo la emoji hizi mpya baadhi ya emoji zilizopo ni pamoja na emoji ya Hijab, mwanamke aliyevaa hijab, mwanaume aliyefuga ndevu nyingi, kichwa cha twiga na nyinginezo nyingi.
Unicode wanajaribu kuzidi kuwa na emoji ambazo zinawakilisha vitu vingi zaidi ili waweze kuwavutia watumiaji wa mitandao kutumia zaidi emoji hizo. Kwa upande mwingine hii ni habari nzuri kwa wanaharakati ambao wamekuwa wanapigania saana usawa katika uwakilishi wa emoji hizi.