Katika ulimwengu wa simu janja katika miaka ya karibu huwezi kukosa kutaja Xiaomi ambao wanaonekana kupendwa na watu wengi maeneo mengi duniani na moja ya rununu ambazo zinaongelewa vyema ni Xiaomi Mi 11.
Simu janja mbalimbali za Xiaomi binafsi zimekuwa zikivutia na hii inatokana na vipengele mbalimbali ambavyo kwa kweli vinavutia hasa kwa yule ambae anapenda kutumia simu janja kwa matumizi mengineyo zaidi ya kupiga/kupokea simu. Si suala la kuongea sana bali simu janja zinaweza kufanya shughuli mbalimbali ambazo hapo awali ilibidi kuwa na kifaa kingine kuweza kufanikisha kazi fulani.
Xiaomi Mi 11 ni simu janja ambayo imetokea kuvutia jicho langu hivyo kufanya kutaka kufahamu sifa zake na si muonekano wake. Hizi ndio sifa za simu janja husika, fuatana nami kuweza kuifahamu:
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.81
- Ubora: AMOLED (1440*2400px, 120Hz); ung’avu wa hali ya juu sana+umbo mithili ya tone la maji kwenye kamera ya mbele
Memori :
- Diski uhifadhi: 128GB/256GB
- RAM: GB 8/12
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 108, 13, na 5+taa mbili za kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 8K, 4K na 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 20+Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px na 720px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4600 mAh
- USB-C 2.0, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 55W (100% kwa dakika 45), kuchaji kwa haraka bila kutumia waya 50W (100% kwa dakika 53), uwezo wa kuchaji simu janja nyingine bila kutumia waya kwa 10W, Power Delivery 3.0 na Quick charge 4+
Kipuri mama :
- Snapdragon 888 5G
Uzito :
- Gramu 196
Programu Endeshi
- Realme MIUI 12, Android 11
Rangi/Bei :
- Bluu, Dhahabu, Kahawia na Nyeupe
- GB 8/128-$586 (zaidi ya Tsh. 1,347,800), GB 8/256-$622 (zaidi ya Tsh. 1,430,600) na GB 12/256-$681 (zaidi ya Tsh. 1,566,300) bei ya ughaibuni
Simu hii ipo sokoni tangu mwezi Januari mwaka huu sasa ni wewe msomaji wetu kuamua iwapo imekuvutia kiasi cha kupanga kwenda kuinunua. Daima usiache kufuatilia TeknoKona ili uweze kuhabarika halikadhalika kuelimika kuhusu teknolojia.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.