Youtube ni jukwaa la kuangalia video mtandaoni na pia kutuma video mtandaoni zenye ukubwa wowote. Jukwaa hili lina wastani wa watumiaji milioni 500 kwa mwezi. Pia jukwaa hili lipo chini ya Google. Watu mbalimbali hutumia youtube kutuma maudhui yao na kulipwa kutokana na vigezo walivyonavyo na wengine huitumia tu kwa kuangalia maudhui ya wengine.
YouTube ilitangaza uamuzi wake wa kufanya idadi ya “kutopenda” kuhesabika kwenye video za faragha kwenye jukwaa lake lote. Uamuzi huo unaweza kuwa wa kutatanisha kutokana na jinsi unavyoathiri mwonekano wa umma katika mapokezi ya video. Lakini YouTube inaamini kuwa mabadiliko hayo yatawalinda vyema waundaji wake dhidi ya unyanyasaji na kupunguza tishio la kile inachoita “mashambulizi ya kutopenda”.
Mabadiliko hayo yanafuatia jaribio lililofanywa na YouTube mapema mwaka huu ambalo lengo lake lilikuwa kubaini ikiwa mabadiliko ya aina hii yangepunguza mashambulizi ya kutopenda na unyanyasaji wa watayarishi. Youtube sio jukwaa pekee lililoamua kufanya uchunguzi wa aina hii hata Facebook na Instagram nao walifanya uchunguzi kuhusu kitufe cha kupenda na wakagundua kuwa inaweza kupelekea watu kutojiamini wanapotumia huduma zao hivyo wamemuwekea mtumiaji uwezo wa kuzuia kitufe chake cha kupenda kisionyeshe idadi ya watu waliopenda.
Chanzo: Techcrunch
No Comment! Be the first one.