Katika mkutano wake na waandishi wa habari, leo kampuni ya Xiaomi imezindua Simu Janja mpya mbili za familia ya Y ambazo zitakuwa na kamera ya mbele (selfie) zenye megapixel 16. Simu janja hizo mbili zilizozinduliwa huko India ni Redmi Y1 na Xiaomi Redmi Y1 Lite.
Kwa mujibu wa kampuni hiyo kameara hizo za mbele zina ubora mzuri na zitakuwa na uwezo wa kuingiza mwanga mkubwa pale picha inapotaka kuchukuliwa. Zitakuwa na flashi kwa ajili ya kusaidia penye mwanga hafifu.
Xiaomi Redmi Y1 na Xiaomi Redmi Y1 Lite zinatumia Android Nougat yenye MIUI 9 Beta ambapo itapata masasisho kuanzia katikati ya Novemba mwaka huu.
Sifa ya Xiaomi Redmi Y1
Mfumo wa Uendeshaji: Android 7.1.2 Nougat yenye MIUI 9 Beta
Kioo: Ukubwa wa inchi 5.5
Prosesa: 1.4 GHz Qualcomm Snapdragon 435 octa-core 64-bit
RAM: 3/4GB
Uhifadhi wa ndani: 32/64GB
Kamera ya mbele: MP 16
Kamera ya nyuma: MP 13
Betri: 3,080mAh
Xiaomi Redmi Y1 itakuwa na aina mbili tofauti ya ujazo wa hifadhi wa ndani na ukubwa wa RAM. Moja itakuwa na 3GB + 32GB ambayo itauzwa kwa Dola 140|Tsh. 314,860 na nyingine ni 4GB + 64GB itauzwa kwa Dola za kimarekani 170|Tsh. 382,330.
Sifa ya Xiaomi Redmi Y1 Lite
Mfumo wa Uendeshaji: Android 7.1.2 Nougat yenye MIUI 9 Beta
Kioo: Ukubwa wa inchi 5.5
Prosesa: 1.4 GHz Qualcomm Snapdragon 425 quad-core 64-bit
RAM: 2GB
Uhifadhi wa ndani: 16GB
Kamera ya mbele: MP 5
Kamera ya nyuma: MP 13
Betri: 3,080mAh
Simu ya Xiaomi Redmi Y1 Lite itauzwa kwa dola za kimarekani 115|Tsh. 258,635. Simu zote mbili unaweza kuweka memori kadi ya kubwa mpaka 128GB.