Mwezi juni niliandika kwamba kampuni ya Xiaomi imejitutumua na kushikilia nafasi ya pili katika soko la kutengeneza na kuuza simu duniani.
Soma Zaidi Makala Yangu Ya Nyuma –> Hapa <–
Ilishika namba hiyo baada ya kuipita Apple ambayo ilikua ikishikilia nafasi hiyo ya pili, huku Samsung ikiwa inashikilia nafasi ya kwanza.
Cha kushangaza ni kwamba Xiaomi mauzo yake yalikua yanakuwa kwa kasi (asilimia kubwa) kuliko kampuni zote kwa wakati huo. Hali ambayo ilipelekea mpaka kampuni kushikilia namba moja hku ya Samsung yakishuka.
Lakini kumbuka katika miezi ijayo tuu kutakuwa na vita kali maana kampuni kama samsung na Apple wanategemea kutoa simu zao ambazo kwa namna moja au zingine zitakua za hali ya juu.
Ni wazi kila mwaka lazima au naweza kusema ni kawaida kwa kampuni hizi kuleta simu janja mpya katika soko….swali linabakia inamaana bado Xiaomi inataweza kuendelea kushika namba moja?
Kingine kumbuka Xiaomi imeweza kushika namba moja baada ya mwaka mzima ambapo Huawei ilikabiliwa na majanga kwani kwa kipindi hicho ilikua inashikilia namba moja katika soko la kuuza na kutengeneza simu duniani.
Taarifa zote ni kwa mujibu wa tafiti iliyofanyika na mtandao wa Counterpoint.. Som Zaida –> Hapa <–
No Comment! Be the first one.