Ni wazi kwamba mara kwa mara tumeweza kuona simu na baadhi ya bidhaa kadha wa kadha kutoka kampuni ya Xiaomi zikiwa na nembo ya ‘Mi’
Msemaji wa Xiaomi amesema kuwa kwa bidhaa nyingi zijazo zitaachana na nembo ya Mi na zitakua na nembo jina ya Xiaomi.
Hii wamedai kuwa itawasaidi katika soko la dunia katika kuhakikisha kuwa soko la dunia linatmabua vizuri kampuni na bidhaa kutoka Xiaomi.
Vile vile kampuni inamesema kuwa kwa sasa bidhaa zenye nembo ya Redmi bado zitabaki kuwepo, hii inamaanisha kuwa kampuni itakuwa na mfumo kama katika picha
Jina la Mi kwa sasa litakua linatumika katika stoo (maduka) za nyumbani (china) kwa wakati huu na pengine hili baadae linaweza likabadilika.
Yote kwa yote ni kwamba tegemea simu janja kutoka Xiaomi kutokua na herufi zile za Mi na bali zitakuwa na jina kamili la kampuni yaani Xiaomi.
No Comment! Be the first one.