Microsoft, watengenezaji wa vifaa vya kuchezea magemu vya XBox wametangaza rasmi ujio wa Xbox Series S pamoja na bei yake.
Microsoft wamesema toleo hilo jipya la Xbox litaingia sokoni Novemba 10 mwaka huu. Kwenye suala la bei itaanzia dola 299 za Kimarekani – takribani Tsh 700,000/=.
XBox Series S inakuja katika rangi nyeupe na inachukua sifa ya kuwa Xbox yenye umbo dogo zaidi, urefu wa inchi 10.8 na upana wa inchi 2.5.
Vingine:
- Inakuja na port mbili za USB.
- Port ya HDMI na Ethernet – kwa ajili ya intaneti.
- CPU ya 3.6GHz, yenye uwezo wa kuhimili uchezaji magemu wa kiwango cha HD cha 1440p na 60fps na zaidi.
- Diski ujazo wa GB 512 pamoja na RAM ya GB 10
Microsoft wanasema Xbox Series S inauwezo wa mara tatu zaidi katika ufanisi ukilinganisha na Xbox One X.
No Comment! Be the first one.