Microsoft katika toleo la kisasa la Window 10 (kuanzia toleo la Oktoba 2018) imewezesha watumiaji wake kuweza kuchomoa kifaa cha USB Flash/Drive kwa usalama bila kufuata hatua ya ‘Safely Remove’.
Microsoft wamesema katika ukurasa wao wa habari kuwa kwa kipindi kirefu kuna machaguo ya aina mbili ya kuchomoa vifaa vya USB kwenye eneo la mipangilio/Setting. Kuna sera/uwezo wa Quick removal na Better performance. Zamani mpangilio wa ‘Better Performance‘ ndio ulikuwa mpangilio mkuu ila sasa inakuwa Quick Removal.
- Quick removal – sera hii itakuwa ya mwanzo kabisa ambayo itawezesha kuchomoa kifaa ya diski uhifadhi cha USB (flash) yako muda wote bila kufanya chochote
- Better performance –sera hii ni nzuri na inaongeza ufanisi na mawasiliano ya kidata kati ya kompyuta na kifaa cha USB Drive/flash. Pia njia hii inahakikisha data zako zinakuwa salama zaidi dhidi ya kuharibika kama wakati imechomolewa kulikuwa na usafirishaji data kati ya kompyuta na kifaa chako cha USB. Lakini endapo mtumiaji akichagua basi itamlazimu kutumia shortcut ya Safe Removely kabla ya mtu kuchomoa kifaa cha usb flash.
picha : microsoft
Sehemu ya kuchagua policy mpya ya kutolea USB FLASH kwenye window
JINSI YA KUWEZESHA SERA HIZI:
- Bonyeza Right Click sehemu ya My Computer/ This Pc alafu chagua Manage
- Alafu chagua Disk Management
- Alafu kwenye sehemu ya usb flash yako (eg, disk *) right click then chagua Properties
- Baada ya hapo sasa unaweza chagua/badalisha chaguzi unayoitaji
MUHIMU : kama unajali kuhusu usb flash yako basi vyema tu kuweka Better Performance