WhatsApp imekuwa ikifanyiwa maboresho ya mara kwa mara amabyo yapo ambayo yameshafika kwa walengwa na mengine bado yanapikwa mfano kuboreshwa kwa mfumo wa kushughulikia yanayoripotiwa kwao.
Unapohudumia watu wengi ama wachache ni vyema ukatafuta namna ya kuwa unapokea mawazo/malalamiko yao kisha kuyafanyia kazi kwa lengo kuboresha na hatimae kuvutia watu wengi zaidi. Ndio, WhatsApp imefanya maboresho madogo kwenye mfumo wake wa yale yanayopelekwa kwao.
Awali, mtu akiripoti kitu WhatsApp basi wenyewe kwa ruhusa yako watapokea nakala ya mazungumzo ya kile ulichokiripoti kwao ili wawe kwenye nafasi nzuri ya kutoa maamuzi, sasa hiyo ilikuwa ni zamani. Katika maboresho ya sasa WhatsApp watapokea jumbe tano tu za karibuni kabisa zitatumwa kwenda kwao ili kuangalia ukweli wa kile ulichokiripoti.
Polepole WhatsApp wameendelea kutafuta namna ya watumiaji kufurahia programu hiyo tumishi ambayo imesheheni zaidi ya watu milioni 2 duniani kote wanaoitumia kila mara.
Yapo mengi ambayo yataletwa kwenye WhatsApp na daima tutaendelea kusaka habari ili kukuhabari wewe msomaji wetu. Je, mara mwisho kupakua masasisho ya WhatsApp ilikuwa lini?
Usisahau kutufuatilia kila siku kupitia mitandao yetu ya kijamii na kwa hakika utajifunza mengi bila kusahau kuhabarika masuala mbalimbali yanayohusu ulimwengu wa teknolojia.
Chanzo: WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.