WhatsApp ni maarufu sana na imekua ikirahisisha mawasiliano kati ya watu kwa muda sasa, pata picha uwezo wa kutuma jumbe za sauti (voice note) katika upande wa status
Ndio, utakua na uwezo wa kuweza kupost jumbe za sauti kama sehemu ya status. Kumbuka kwa sasa inawezekana picha, video na jumbe za sauti tuu lakini hilo linaenda kubadilika
Tumeona kwa kipindi cha muda mfupi, mtandao huu wa WhatsApp umeweza kuja na masasisho mbalimbali huku na vipengele vipya kede kede.
Hapa kinachotokea ni kwamba mtandao wa WhatsApp utakuwezesha wewe kuweza kurekodi jumbe za sauti (kwa haraka) na kuweza kuzituma katika eneo la Status Katika App hiyo.
Hapa hakuna tofauti sana na kutuma jumbe za suati kwa watu mbalimbali kinachobadilika ni kwamba hii unatuma katika eneo la status.
Kipengele hichi kwa sasa kipo katika hatua za mwanzo mwanzo kabisa za utekelezaji, lakini ni moja kati ya vipengele vinavyo subiriwa kwa hamu sana.
Ukiachana na yote haya, bado haijulikani ni lini kipengele hichi kitakapoanza kutumika na kufikia watu wote
Ningependa kusikia kutoka kwako, nianidikie hapo chini katika eneo la comment, je uko tayari kaunza kutumia kipengele hichi?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.