WhatsApp imekua na maboresho/masasisho (Update) nyingi sana katika siku za karibuni, lakini fikiria uwezo wa kutoka kwenye group kimya kimya.
Hii kwa namna moja au nyingine inamaanisha kuwa mwana kikundi (Group) anaweza akajitoa kimya kimya katika group husika bila ya mtandao wa WhatsApp kutaarifu kila mwanachama katika Group hilo.
Kumbuka mpaka sasa WhatsApp wanaruhusu makundi hadi ya watu 256 katika mtandao wao, kumbuka watu wakishakua wengi hivyi katika kundi lazima kutakua na mambo mengi sana.
Hapa inabidi ufikirie maana hata watu wakiwa wachache saa zingine inakua ni shida kidogo sio?
Ukichana na uwezo huo vipi kuhusu uwezo wa kuona link kwa ukubwa wake katika eneo la ‘status’ –yaaani hapa hata baadhi ya ‘preview’ –tena kwa ukubwa– zitaweza onekana.
Kwa sasa WhatsApp wenyewe hawajaweka wazi kwamba ni lini vipengele hivi vinaweza kupatikana kwa watu
CHANZO: wabetainfo
Niandikie hapo chini katika eneo la comment hii umeipokeaje? ningependa kusikia kutoka kwako.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.