kipengele hiki kipya kutoka WhatsApp kinakuwezesha kujiunga katika kundi la watu ambao wanaongea kwa kupitia huduma ya simu za kuonana ndani ya mtandao huo.
Uzuri wa hii ni kwamba hata kama watu wameshaanza kuongea labda wapo wanne na wewe unaweza ukaongezeka na ukawa watano.
Uzuri wa hii ni kwamba utaweza kujiunga na mazungumzo hayo wakati ukiwa tayari kwa ridhaa yako mwenyewe, huduma hii inafanana na Zoom na hata Google Meet.
Kwa ukubwa ambao mtandoa wa WhatsApp unao kipengele hichi kitakuwa ni kikubwa sana maana mtandoa unapatikana kwa kiaisi kukubwa kuliko mitandao mingine ambayo unafanya huduma inayofanana.
Pata Picha Kwanza…
Ushapata Picha Sio?
Vile vile unaweza kuona kwamba nani na nani wamealikwa kwenye mazungumzo hayo na wakina nani ambao wamealikwa lakini bado hawajajiunga na mazungumzo hayo.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini sehemu ya comment nini maoni yako kuhusu hili.
Kumbuka Kutemebelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
No Comment! Be the first one.