WhatsApp haitafanya kazi 2021 katika simu kadhaa zinazotumia Android na iOS. Sababu zikiwa ni za kiusalama na za kiteknolojia.
Ni kawaida kila baada ya miaka kadhaa kwa WhatsApp kuacha kufanya kazi au kutotolewa kwa matoleo mapya/masasisho kwa baadhi ya simu.
Mara nyingi sababu kuu huu ni simu hizo kufikia mwisho wa kupokea masasisho (updates) ya programu endeshaji (os).
WhatsApp ni moja ya app maarufu duniani na moja ya app muhimu kwa watumiaji wa simu janja za aina zote, iwe Android au za iPhone.
Kwa iPhones
Simu za iPhone zinazotumia programu endeshaji ya iOS ya chini ya toleo la 9 (iOS 9) zote zitakosa kupata app ya WhatsApp tena. Kwa sasa hii ina maanisha simu za iPhone 4 na nyingine zote zilizotoka kabla yake.
Kwa watumiaji wa simu za 4S, 5, 5S, 5C, 6 na 6S watatakiwa kuhakikisha wanatumia toleo la iOS 9 au jipya zaidi ili kuweza kuendelea kutumia app hii maarufu ya mawasiliano.
Kwa simu za Android
Kama simu unayotumia ina toleo la Android la 4.0.2 na nyuma basi itakuwa ndio mwisho wa kuweza kutumia app ya WhatsApp. Simu ambazo hazina uwezo wa kupata toleo la Android la juu zaidi ya hapo ni pamoja na HTC Desire, Motorola Droid Razr, na Samsung Galaxy S2. Simu hizi hazitakuwa na uwezo tena wa kutumia app ya WhatsApp.
Je utahakikishaje kama simu yako ipo salama?
Hakikisha simu yako inatumia toleo la kisasa la programu endeshaji (OS).
Jinsi ya kuangalia toleo la programu endeshaji la simu yako.
iPhone:
Bofya Settings > General > Information
Hapo utaona kuhusu taarifa za toleo la programu endeshaji yako.
Android:
Bofya Settings > About System/Device
Hapo utaona taarifa kuhusu toleo la programu endeshaji yako.
Soma makala na maujanja ya WhatsApp -> Teknokona/WhatsApp
My phone tekno fg lite Android 8.0 je itafungiwa kutumia watsaap?