Hadi sasa kama ni mtu wa mitandao ya kijamii basi utakuwa umekwishaona taarifa ya kwamba apps za WhatsApp, Facebook na Instagram zapata shida inayosababisha mamilioni ya watumiaji wake kushindwa kupata huduma iliyo bora kwa sasa.
Watumiaji walioathirika wameshindwa kudownload picha, video n.k hasa kwenye jumbe za WhatsApp ila ata wa Instagram na Facebook wamepata shida hiyo hiyo.
Nini kimesababisha;
Tatizo limetokea kwenye baadhi ya kompyuta mama za data (Servers) zinazomilikiwa na Facebook ambazo zinahudumia huduma hizi zote tatu.
Maeneo yaliyoathirika;
Kwa Tanzania tatizo lipo ingawa si ukubwa sana; ila tayari wapo ambao wanaathirika, tatizo kubwa limekuwa barani Ulaya na Amerika ya Kusini. Mitandao inayohusisha huduma za kutambua okosekaji wa huduma za kimitandao imeweza kutoa data ambazo zinaonesha mataifa yaliyoathirika zaidi;
Angalia picha hii, kwenye wekundu zaidi ndio kwenye shida zaidi kwa wingi wa watumiaji ambao wameshindwa kupata huduma za apps hizi kwa sasa.
Hii si mara ya kwanza na kwa huduma za kimtandao ni jambo ambalo hutokea, ila kwa Facebook inawezekana ikawa ni muda wa kujitazama na kufanya maamuzi ya kuboreshwa kwani ni mwezi wa tatu tuu huduma hizo tatu zilipitia matatizo haya haya. Na kwa kila dakika ambayo huduma hizi zinakuwa zinapata shida kampuni hiyo hupoteza mapato mengi kutokana na kushindwa kurusha huduma ya matangazo.
Soma habari mbalimbali kuhusu apps mbalimbali -> Teknokona/Apps