Watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini Uganda sasa watatozwa ushuru mpya ili kuzuia kile ambacho rais Yoweri Museveni anataja kama “Lugambo” (umbea).
WhatsApp, Facebook, Twitter, Skype na Viber ni miongoni mwa mitandao inayolengwa kwakua ndio hutumiwa na raia wengi nchini Uganda. Inadaiwa kuwa hatua hiyo imechukua kutokana na kile ambacho serikali inadai “Ni tabia ya wananchi kuitumia mitandao hiyo kuikosoa serikali bila sababu yoyote”.
Rais Museveni pia analenga kuwatoza kodi zaidi wamiliki wa majengo ya kibiashara katika jitihada za kuimarisha mapato ya serikali kando na UGSh. 50 bilioni ambazo hukusanywa kutoka kwa wamiliki wa nyumba kila mwaka.
Watumiaji mitandao ya kijamii wamekashifu hatua ya serikali kuaza kutoza mitandao ya kijamii ushuru zaidi huku watetezi wa haki na viongozi wa upinzani wakidai hatua hiyo inahujumu haki za watu. Vilevile, wanalalamika kuwa ongezeko la ushuru ni mzigo kwa wananchi.
Ongezeko la ushuru kwa mitandao ya kijamii
Chini ya mpango huo, serikali ya Museveni inapania kukusanya Sh. 400 bilioni (za Uganda) na Sh. 1.4 trilioni (za Uganda) kutoka kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii.
Pia, vitawekwa viwango vipya vitawekwa kwa ajili ya watumiaji intaneti kwa shughuli za masomo na utafiti na huduma hizo hazitakuwa zikitozwa ushuru wowote.
Hata hivyo, “Olugambo” katika mitandao ya kijamii (yaani maoni, matusi, kupiga soga) na matangazo ya kampuni ya Google vitatozwa kodi. Chini ya mpango huo watumiaji wa WhatsApp, Skype, Viber, Twitter, n.k watatozwa ada ya UGSh. 100 kila siku na kuiwezesha serikali kukusanya UGSh. 400 bilioni zaidi kila mwezi.