Siku hazilingani na kila kitu kina changamoto zake. Watumiaji wa soko la Coinbase wameonja shubiri ambayo haikutegemewa hata kidogo na hii inafuatia mara baada ya kupokea ujumbe uliowashtua.
Daima teknolojia haijaacha kuwa na panda shuka kwa maana ya changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikipatiwa ufumbuzi. Coinbase ni soko la sarafu za kidijitali lenye makao yake makao yake makuu huko Wilmington, Delaware-Marekani limejikuta mahali pabaya baada ya ujumbe uliokuwa umetumwa kimakosa kwa njia ya barua pepe ukiwataarifu watumiaji wake mfumo wa kutumia njia mbili za kuhakikisha usalama umebadilishwa!
Kwa muda wa dakika 82 watumiaji wa soko hilo la sarafu za kidijitali walipokea ujumbe ambao ulikuwa si mzuri kwa muktadha wa usalama pesa zisizoshika lakini pia biashara kwa upana wake. Ujumbe huo uliwaataarifu wateja kuwa mpangilio wa kutumia njia mbili za kuweka ulinzi umebadilishwa. Ujumbe huo ulitumwa kimakosa kutokana na changamoto za ndani kwa ndani na halikuwa pengine wamedukuliwa.
Madhara yaliyosababishwa na ujumbe uliotumwa kimakosa
Mbali na kusababisha taharuki kwa watumiaji wa soko hilo la lakini pia haikuwa rahisi kutuma ujumbe kwa watu wote mara moja kuwataarifu kuwa ujumbe waliopokea kwenye barua pepe zao ulitumwa kimakosa hivyo ikabidi watumie ukurasa wao wa Twitter kuwataarifu kilichotokea halikadhalika kuwa suala hilo limeshawekwa sawa.
Our teams immediately recognized the problem and worked as quickly as possible to ensure these erroneous notifications were stopped and the underlying issue fixed.
— Coinbase (@coinbase) August 28, 2021
Ujumbe huo uliokuwa umetumwa kimakosa uliwafikia watu wapatao 125,000 na hata kusababisha baadhi ya watu haraka haraka kuuza sarafu zao za kidijitali zenye thamani ya $600,000 kwa hofu ya kuzipoteza kwa wadukuzi. Je, wewe ulikutana na ujumbe huo?
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.