Kukatazwa kutembelea tovuti fulani kwenye kifaa cha kidijitali inafanya watu kutafuta njia mbadala ya kuweza kuperuzi bila kuweza kujulikana na hapo ndipo matumizi ya VPN yanakuja sehemu yake ambapo watumiaji wa Google One wana uwezo wa kuzunguka huku na kule mtandaoni kwa uhuru.
Memori za kwenye simu janja zinaweza zisitoshe kulingana na matumizi ya mtu mwenye hivyo kusababisha kutafuta nyongeza ili ipatikane nafasi ya kuhifadhi data zake akiwa na uwezo wa kuzifikia mahali popote na wakati wowote. Google ni huduma ya kulipia kwa mwezi/mwaka ambayo ina mtu uwezo wa kununua memori kuanzia GB 100 hadi TB 2.
Kwa muda mrefu wanaotumia Google One kwenye iOS wamekuwa wakikosa huduma ya VPN mpaka hivi karibuni ambapo mtu akinunua memori ya TB 2 basi mbali na faida nyinginezo ambazo zinakuja pamoja na huduma hiyo pia watumiaji wake wataweza kutumia VPN.
Huduma hiyo ya Google pia ina kipengele kipya ambacgo kinaruhu mtu kuondoa intaneti kwa usalama iwapo VPN imewashwa na kuwezesha baaddhi ya programu tumishi intaneti ya kawaida badala ya VPN. Huduma hii ya VPN inamuwezesha kuweza kuruhusu na wana familia mpaka watano kuweza kuitumia bila gharama ya ziada.
Je, imeshapatikana kote duniani?
Huduma hii imeshaanza kupatikana kwenye nchi kadha wa kadha zikiwemo Austria, Belgium, Denmark, Finland, Iceland, Ireland, Uholanzi, Norway, Sweden na Switzerland huku kuzidi kwenye mataifa mengine kadri muda unavyosogea. Kuhusu usalama wake Google wamejinasibu kwamba wameweka ulinzi wa hali ya juu katika kufanikisha watu wanaperuzikwa usiri wa aina yake.
Kwenye dunia ya leo matumizi ya VPN yanaonekana kukua na ni wazi kuwa zipo programu tumishi, vivinjari, n.k ambazo zimetengenzwa kwa kuwekwa kitu hicho. Je, wewe ni mmoja ya wale ambao hupenda faragha unapoperuzi mtandaoni?
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.