Inawezekana kabisa ukawa miongoni mwa watu ambao hawaamini katika mawasiliano ya kupitia picha jongefu (mnato/video) lakini wakati huu ambao dunia inapambana na virusi vya COVID-19; teknolojia hiyo ndio mkombozi wa wengi ukiacha Skype, WhatsApp na hata kwenye Google Duo.
Google ni moja ya makampuni ambayo huwa hayaoni hiyana kuachana na kitu kama wanaona hakina watumiaji wengi/umaarufu wake umeshuka. Mwezi Agosti 2016 kampuni hiyo iliruhusu programu tumishi iitwayo Google Duo kuweza kupatikana kwenye App store au Playstore kwa simu janja zenye Android 4.1 kuendelea ama iOS 9 kwenda mbele. Na tangu wakati huo imekuwa hewani. Kufahamu zaidi kuhusu Google Duo BOFYA HAPA.
Teknolojia ya kutumia picha mnato kufanya mawasiliano wakati kila mtu akiwa kwake kwa usaidizi wa intaneti imekuwa ni jibu sahihi katika kuhakikisha watu hawakusanyiki kujadili mambo ana kwa ana ili kuepusha kuenea kwa virusi vya Corona vinavyosababisha homa ya mapafu. Google wameona inafaa kuiongozea uwezo programu tumishi husika kutoka watu wanane (8) wanaoweza kuwasiliana kwa wakati mmoja hadi kumi na wawili (12).
Ndio, hivyo ambavyo ambavyo umuhimu wa kutumia teknolojia ya kuonana kupitia bidhaa za kielekroniki ukiongezeka wakati huu ambapo serikali za nchi nyingi zimeamrisha watu wake wakae majumbani.
Vyanz0: 9To5Google, GSMArena
One Comment
Comments are closed.