Watu wengi tuu duniani wameonekana kuwa na nia ya kutaka kutumia Windows 11 wakati sahihi utakapofika kwa maana ya kuzinduliwa rasmi na Microsoft. Katika kufanya mambo yavutie Microsoft imesema haizuia kompyuta za zamani kuiweka programu hiyo endeshi.
Nina amini wale ambao tunatumia kompyuta ambazo ni toleo la nyuma tuna wasiwasi kama kompyuta zetu zipo kwenye orodha ya zile ambazo zinaweza kuweka Windows 11. Microsoft wameliona hilo na kuamua mambo wazi kwamba hata wale ambao kompyuta zetu ni za zamani bado tunaweza tukaishusha na kuiweka kwenye vifaa vyetu.
Windows 11 kutobagua kompyuta
Kwa taarifa iliyopo kwa kompyuta zote ambazo Microsoft inaona zinafaa kuhamia Windows 11 zitapokea taarifa fupi ya kumjulisha mtumiaji kuwa anaweza kuishusha na kuiweka kwenye kifaa chake katika mtindo wa kupakua masasisho. Hata hivyo, wale ambao tuna kompyuta toleo la nyuma tunaweza tusipate hiyo taarifa fupi lakini mtu mwenyewe anaweza kuingia mtandaoni na kuishusha kisha kuiweka kwenye komyuta.
Lakini nguli hao kwwenye masuala ya kompyuta wamebadilisha mawazo na kueleza kuwa toleo hilo litakuwa kwa kompyuta hata zile za zamani kwa lengo la kupata maoni kuhusiana na programu hiyo endeshi.
Ingawa kwamba toleo hilo la programu endeshi litapatikana katika kompyuta nyingi zaidi lakini ujue kuwa utaishusha huku bila kujua iwapo itaendana na viwezeshi (drivers) au vingninevyo ndani kompyuta yako na kama haziendani itakuwa ni hasara kwako kwani itakulazimu uitoe.
Vyanzo: The Verge, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.