HalloApp ni mtandao wa kijamii wenye sifa ya kipekee ukilinganisha na mitandao mingine, mtandao huu umeanzishwa rasmi na wafanyakazi wawili wa (mwanzo) zamani kabisa wa WhatsApp.
Mtandao huu wa kijamii kwa sasa unapatikana Apple’s App Store na Google Play
Dhima nzima ya mtandao huu ni kuwaunganisha karibu zaidi watu wa kundi ambalo wanafahamiana vizuri kama vile marafiki na familia
Kama WhatsApp tuu ili kuweza kuwasiliana na watu hao lazima uwe na namba zao za simu ili kuweza kufanikisha maongezi nao katika HalloApp.
Meseji ambazo zinatumwa na kupokelewa zinakuwa na usalama wa hali ya juu (encrypted) na vile vile kunakuwa hakuna matangazo ya aina yoyote ndani ya mtandao huo.
Somewhere along the way, social media went seriously wrong.
• What we post is rarely who we are.
• What we see isn't from people we know.
• What we talk about online isn't what we talk about in private.Where can we be ourselves?
🧵👇
— neeraj arora (@neerajarora) July 19, 2021
Wawili hao nyuma ya mtandao huo ni Neeraj Arora na Michael Donohue amabo wote walikua katika nafasi za juu za WhatsApp kabla haijanunuliwa na Facebook.
Kwa sisi TeknoKona tunapenda kuona mtandao huu unazidi kukuwa na kuleta mapinduzi makubwa katika mitandao ya kijamii katika kuhakikisha tunapata huduma bora zaidi
No Comment! Be the first one.