Matumizi yetu ya kila siku kwenye simu/kifaa chochote kinachotumia nguvu ya betri yanasababisha kuisha kwa chaji hivyo basi kutakiwa kujazwa umeme ili kuweza kufanya kazi. Lakini pia kutokana na ukuaji wa teknolojia na utandawazi kwa ujumla wake wadukuzi wanaweza wakasababisha kitu kikaishiwa chaji bila hata ya kuelewa na ukafikiri betri la kwenye kifaa husika lina tatizo.
Katika akili ya kawaida tu hata kama si mjuzi/mfuatiliaji wa masuala ya teknolojia simu au kifaa cha kidijiti kikiwa hakitunzi chaji kwa muda mrefu wengi wetu huwa tunafikiri ni betri lenye lilivyotengenzwa ndio lina tatizo au tukienda mbali kidogo ni kutokana na programu ambazo zipo kwenye kifaa husika ndio zina maliza chaji, sikatai lakini pia wadukuzi wana nafasi yao kuweza kumaliza chaji kwenye bidhaa za kidijitali, nitaeleza kwanini.
Juzi juzi tu kuna kundi la wadukuzi limebainika kwa udanganyifu ambao unasabisha kumaliza chaji kwenye simu janja au bidhaa nyinginezo za kidijitali, wanafanyaje? Kwa kutumia programu fulani wanakuonyesha tangazo moja la kitu fulani lakini nyuma ya pazia kuna matangazo mawili na zaidi yanafanya kazi kitu ambacho kinanyonya betri.
Lakini pia watu hao wanaweza wakalipia tangazo la bidhaa fulani ili kuweza kujulikana na hata kutembelea tovuti husika kuweza kufahamu zaidi na baada ya tangazo hilo kuletwa kwa mlaji linagawanywa mara tatu (3) au zaidi bila ya mteja kujua na kuuzwa kwa bei ya juu kitu ambacho kinafanya mdukuzi kuingiza pesa zaidi.