Toleo la Android 12 ndio habari ya sasa ambayo inaanza kwenda kwenye simu janja ambalimbali duniani katika mpango ambao kampuni zilizotengeneza rununu husika imejiwekea. Samsung ni mojawapo ya kampuni ambazoimeshaweka ratiba ya simu zitakazopokea taarifa kuhusu kuhamia kwenye toleo hilo.
Vionjo vya Android 12 vimeanza kuonekana kwenye Samsung Galaxy Z Flip 5G smbspo imeanzia kwa wenye simu hizo nchini Marekani. Jambo hili limepokelewa katika mtazamo chanya kwani wenye simu hizo wanapata kuona mwonekano wa vitu kwenye simu zao hata kabla ya programu yenyewe endeshi kuanza kupatikana kwa watumiaji wote.
Vionjo hivyo vya muonekano wa Android 12 kwenye Samsung Galaxy Z Flip 5G vitambulika kwa utambulisho wa aina yake-F707U1UEU2EUL9 na F707USQS2EUL9 kwa ajili ya toleo jingine la simu janja husika.
Masasisho hayo ambayo yanatoka sambambamba na yale yanayohusisha suala zima la kufanya simu janja ziwe madhubuti kwa mwezi Disemba 2021. Halikadhalika, inaelezwa kuwa tayari Samsung wameshaanza kutoa masasisho ya ulinzi kwa mwezi Januari 2022.
Vionjo hivyo vya Android 12 kwenye Galaxy Z Flip vimeanzia Marekani na tayari Samsung wameshaweka wazi ratiba yake kuhusiana na mpango wa kupeleka toleo hilo jipya la programu endeshi kwenye rununu mbalimbali za kampuni hiyo. Salia nasi na tutaileta makala hiyo mbele ya macho yenu.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
One Comment