Hii imekua ikiwatesa wengi maana kwa kawaida ukiwa unaangalia video katika mtandao wa youtube na kisa ukawa unataka kufanya kitu kingine (kufungua App nyingine kwa mfano) ulikua unashindwa mpaka utoke kabisa Youtube.
Hii inamaana kuwa kama unatazama video na unataka kutuma meseji inabidi uchague kitu kimoja aidha kutuma meseji au kuendelea kufurahia kuangalia video hizo katika App ya youtube.
Hili wameliona na kwa sasa wanashughulikia maana wana mpango wa kuja na kipengele kinachoitwa picture-in-picture kipengele hichi kitakua katika iOS kwa maana ya App (Youtube) za iPhone na iPad.
Hapa inabidi kuwa na uvumilivu kidogo maana kipengele hichi kitaanza kupatikana kwa wale ambayo wanatumia huduma ya kulipia kutoka Youtube inayojulikana kama Youtube Premium.
Baada ya muda ndio itaanza kupatikana mpaka kwa wateja ambao wanatumia mtandao wa Youtube bila malipo ya msimu.
Bado simu maalumu ambayo kipengele kitaanza patikana haijawekwa wazi.
CHANZO: The Verge
Je unasubiria kwa hamu kipengele kama hiki au unaona hakina maana sana kwa sasa? ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Pendwa Wa TeknoKona Kila Siku Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
No Comment! Be the first one.