Siku hizi kuna mtindo kwenye WhatsApp unaweza kutumia kitu na mtu kisha baada ya muda fulani kinakuwa kimetoweka na si kwamba kimefutwa la hasha! Ila ni maboresho tuu ambayo yanatazamuwa kufika hadi kwenye jumbe ndani ya makundi/watu wote.
Watumiaji wa WhatsApp tutarajie kukutana na maboresho ambayo yanahusisha sura mya ya suala zima la jumbe kutoweka. Fahamu ya kuwa wataalamu wanasuka maboresho ambapo ule uwezo wa kitu ambacho umemtumia mtu kupotea baada ya siku sababu sasa unaboreshwa kutoka kwa mtu mmoja moja hadi kwa watu wote na makundi pia.
Kwa mujibu wa WaBetaInfo, inaonekana siku za mbeleni wakati ambapo watumiaji watapokea taarifa ya kutakiwa kupakua masasisho yanayohusu WhatsApp basi watakutana na kipengele kipya ambcho kinampa mtumiaji uwezo wa kuweka mpangilio wa kile anachokituma kutoweka baada ya muda fulani.
Je, kipengele hicho kimeshaanza kuonekana?
Ukweli ni kwamba kipo kwenye hatua za kutengenezwa hivyo majaribio yako ni kwa watu wachache sana ambao wanakuwa wanapewa uwezo wa kujaribu vitu ambavyo vinaboreshwaq kabla ya kuletwa kwa watumiaji wote ingawa kimsingi wote wanaotumia WhatsApp Beta kote kwenye Android na iOS wanapata fursa ya kuona na kutumia yale ambayo yameboreshwa kabla ya wengine iwapo wanatumia toleo la karibuni kabisa kwa wakati huo.
Tuambie ewe msomaji wetu je, unapendezwa na kipengele cha jumbe kutoweka kwenye WhatsApp? Tuandikie maoni yako hapo chini.
Chanzo: WABetaInfo
2 Comments