WhatsApp ina watumiaji wengi zaidi duniani zaidi ya programu tumishi yoyote kwa sasa na mara kwa mara imekuwa ikifanyiwa marekebisho kuifanya kuwa nzuri maradufu. Huko mbele tusije kushangaa kuwa na uwezo wa kutengeneza kijiji ndani ya WhatsApp.
Habari zilizopo huko mbele tutaweza kutanua wigo wa kuwafikia watu wetu kwa rahisi wote wakiwa sehemu moja kwani zipo taarifa kuwa kuna kitu kinachoitwa “WhatsApp Communities” ambacho kwa sasa kipo katika hatua za utengenezwaji.
WhatsApp Communities ni nini?
WhatsApp Communities ama kwa mujibu wa tafsiri isiyo rasmi “Jumuiya za WhatsApp” hapa ni sehemu binafsi ambayo viongozi wa makundi mbalimbali watakuwa na uwezo wa kuleta makundi yote sehemu moja hivyo kuweza kuyaongoza vizuri.
Faida kubwa ya kuwa na “Jumuiya” ndani ya WhatsApp ni nini?
Faida ya jumuiya ndani ya WhatsApp kimsingi ni uwezo viongozi wa makundi kuweza kuwafikia watu wake (kutengeneza kijiji) kwa urahisi zaidi kwani wakiandika ujumbe na kuutuma utafika kwa watu wote mara bila ya kuhamahama kuwenda kutuma ujmbe kwenye makundi mengine.
Kipengele hiki bado hakijafika kwenye toleo la majaribio upande wa Android au kwingineko kokote kwani bado kinawekwa sawa na waundaji ila upo uwezekano wakukiona kwenye maboresho yatakayotolewa huko mbeleni.
Chanzo: WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.