Kama ambavyo ilivyo mitandao ya kijamii mingi tuu kwamba unaweza kumtaja mtu kwenye kile ambacho umekiandika kwa maana ya wengine kuweza kuona vivyo hivyo kwenye Twitter inawezekana pia. Halikadhalika, hata kujiondoa kwenye mazungumzo inawezekana.
Waliopo kwenye kitendo cha kufanya maboresho kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter wamekuwa wakileta maboresho mbalimbali katika miezi ya karibuni kitu ambacho ni kizuri na kuweza kusababisha watu wengi kutumia Twitter. Sasa unaweza ukapatisha kitu chako kwenye Twitter na kuamua kutaja mtu/watu au jina la shirika/kampuni na sote tunajua mhusika atapelekewa taarifa fupi kuwa ametajwa kwenye chapisho lako lakini pia kuwezakutembelea kusoma/kuona hicho ambacho umekiweka.
Katika suala zima la kutaja watu/mashirika au makampuni kwenye Twitter sasa kuna majaribio yanafanyika ambayo yanamuwezesha yule aliyetajwa kuweza kujiondoa kwenye chapisho. Iwapo unakuwa hujapendezwa kutajwa kwenye chapisho au hutaki tena kuendelea kupata taarifa fupi kuhusiana na maoni ya watu mbalimbali kuhusiana na chapisho husika basi inawezekana kujiondoa hivyo kufanya usijue tena kinachoendelea kuhusiana na chapisho ulilotajwa.
Unapoamua kujiweka kando kuhusu kinachoongelewa ndani ya Twitter basi jina lako halitaonekana kuwa na kiunganishi (hyperlink) bali litakuwa la kawaida tuu kama ambavyo ungeandika neno lolote lile. Kwa lugha nyingine kitendo cha wewe kujitoa kuhusu kinachozungumzwa ndani ya Twitter ni ishara kwa yule aliyekutaja kuacha kukutaja kwenye machapisho yake yajayo.
VyanzO: Gadgets 360, mitandao mingine
No Comment! Be the first one.