Ushirikiano kati ya Vodacom Tanzania na Mdundo.com umekuwa ukipikwa kwa muda sasa na hatimae wawili hao wamefikia makubaliano ya kufanya kazi pamoja.
Mdundo ambao wanamiliki tovuti (mdundo.com) halikadhalika programu tumishi inayopatikana kwenye App Store/Playstore mahususi kwa ajili ya huduma za muziki kutoka kwa wasanii mbalimbali ndani na nje ya Afrika wameamua kuunganisha nguvu zao na Vodacom Tanzaia katika nyanja ya kupeleka burudani kwa wananchi.
Vodacom Tanzania imeanzisha kifurushi cha muziki ambacho wateja wake wanaweza kununua ili kuweza kusikiliza/kushusha nyimbo zilizo kwenye kipengele cha kulipia ndani ya mdundo.com (tovuti/programu tumishi).
Kwanini Vodacom Tanzania na Mdundo.com?
Vodocom Tanzania imekuwa kampuni ya mtandao wa simu iliyo na wateja wengi kuzidi kwa wengine ambapo takwimu zinaonyesha kuwa wana wateja zaidi ya milioni 15. Kwqa upande wa Mdundo.com wenyewe wana wateja zaidi ya milioni 7 wa kila mwezi Afrika nzima.
Kitu kingine ambacho kimesaukuma ushirikiano huo ni kutyaka kufanya watu kwenda huku na kule kutafuta nyimbo za miondoko mbalimbali hivyo ukaonekana ulazima wa kuwavutia wateja wa Vodacom Tanzania, Mdundo.com na wengineo kwa namna yake.
Ushirikiano huo unafanya mdundo.com kuwa na nyimbo za miondoko yote sehemu moja ambapo mteja wa Vodacom Tanzania anaweza kuzisikiliza kwa kifurushi cha siku-Tsh. 100, wiki-Tsh. 500 na mwezi-Tsh. 3,000 ambapo mteja ataweza kupata huduma ya muziki kwa kulipa ndani ya programu tumishi husika.
Mdundo.com inaonekana kukua kwa kasi nchini Tanzania jambo ambalo limewafanya Vodacom kuwa kampuni ya kwanza kuamua kufanya nao kazi. Haya sasa ewe msomaji wetu kazi kwako. Je, habari hii itakufanya kuwa mteja wa Vodacom/mdundo.com?
Vyanzo: Techcabal, Mdundo.com
No Comment! Be the first one.