Kadri siku zinavyokwenda na watu/makampuni mbalimbali yanazidi kuleta teknolojia zinazovutia, zenye ubunifu wa aina yake. Utakuwa umeshawahi kusoma makala zetu kuhusu vioo vinavyojikunja lakini kuna mshindani mwingine katokea.
Teknolojia/ubunifu ni moja ya vitu ambavyo havina mipaka na hivyo basi kampuni moja yenye makao yake jijini California, Marekani imeonekana kuwa kivutio kwa wengi kutokana na kile ambacho imetengeneza.
Royole imetengeneza kioo cha kutumika kwenye simu rununu ambacho kinaweza kujikunja na kuvaliwa kwenye mkono kama bangili.
Kampuni hiyo imeshafanya kazi na makampuni mbalimbali kutengeneza vioo vyenye teknolojia ya kujikunja kuanzia kwenye magari, spika, n.k. Washindani wengine ambao wanaonekana kuweka teknolojia hiyo ni Samsung, LG, Lenovo.