TCRA ilisitisha kwa muda suala la usajili wa leseni za maudhui mtandaoni tangu Januari 28 ili kuboresha vitu fulani fulani lakini sasa wameanza tena kupokea maombi.
Nchini Tanzania kuwa na “Leseni za maudhui mtandaoni” ni kiutu muhimu sana kwa yeyote yule ambae anafanya shughuli za kuhabarisha watu kwa njia za kidijiti na kufuatia tamko la hivi karibuni kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuhusu vyombo ya habari vilivyofungiwa na serikali TCRA imeamua kufungua milango na kupokea maombi ya leseni za maudhui mtandaoni.
Usitishwaji huo ambao ungedumu mpaka Juni 30 lakini sasa maombi ya leseni hizo za maudhui mtandaoni yameanza kupokelewa tangu Aprili 9 2021 na hivyo basi kwa wale ambao watakuwa wamekidhi vigezo kwa mujibu wa kanuni WATARUHUSIWA.
TCRA wanasema kuna kazi ya kitaalamu imefanyika ili kuhakikisha tunasimamia vyombo hivyo ndiyo maana wameondoa zuio.
Kuhusu tozo/ada za leseni za maudhui mtandaoni zenyewe zipo palepale kwa sababu zimewekwa kwa mujibu wa sheria na kanuni kama itakuwa vinginevyo basi itategemea na wizara itakavyoamua.
Haya sasa shime kwa wote ambao tunajishughulisha na masuala ya mtandaoni tupeleke maombi yetu ya kupata leseni lakini kikubwa zaidi tujitathimini kama tunakidhi vigezo kulingana na kanuni zilizowekwa.
Vyanzo: Gazeti la Mwananchi, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.