Ni jambo la kawaida sana mtu kusogeza mbele au kurudisha nyuma video kwenye YouTube na kutokana na maboresho mbalimbali jambo hilo wala halijifichi kwani wahusika wanaboresha mambo mara kwa mara.
Uwezo wa kumuwezesha mtu kurusha/kurudisha nyuma video kwenye YouTube umekuwa ukiboreshwa mara kwa mara na ambapo hivi sasa kuna manmna mpya ya watumiaji wake wa kwenye simu janja (Android/iOS) kuweza kurusha ama kurudisha nyuma picha mnato.
Tunafahamu kuwa ile njia ya kusogeza mbele/kurudisha nyuma video kwa sekunde kumi, si ndio? Basi fahamu ya kuwa kipengele hicho kipo katika hatua ya majaribio kwa kuwezesha watumiaji kupangusha kwenda upade wa kushoto ama kulia ili kuweza kurudisha nyuma/kupeleka mbele picha jongefu kwa upande wa simu.
Je, kipengele hicho kinaonekanaje?
Kwanza kabisa kingele hicho kipo katikati ya uso wa mbele wa YouTube ya kwenye simu janja na wakati wa kuanza kuangalia video husika si rahisi kujua jinsi ya kusogeza mbele/kurudisha nyuma picha mnato lakini ukigusagusa kwenye uso wa mbele tu basi itatokea alama ambapo mbele yake yapo maneno yanayosomeka “Slide left to right to seek” kwa maana ya “Sogeza kwenda kulia ama kushoto kuweza kupeleka mbele au kurudisha nyuma na hata kurukisha kabisa”.
Wanaotumia YouTube Beta toleo namba 16.31.34 upande wa Android wameweza kukiona na kukitumia kipengele hicho kipya ambacho kinalenga kurahisisha watu kuwea kupeleka/kurudisha nyuma video. Halikadhalika, baadhi ya wanaotumia iOS wameweza kukiona pia.
Kipengele hicho kipya ndani ya programu tumishi mahususi kwa ajili ya picha jongefu upande wa simu janja bado hakijaanza kuapatikana kwa wote lakini tutegemee kukiona kwenye vifaa vyetu katika siku za usoni.
Vyanzo: Gadgets 360, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.