Upimaji tezi dume umekuwa ni moja ya jambo ambalo bado limekuwa likifanywa kwa njia ambayo imewafanya wanaume wengi kutokuwa na mwamuko katika upimaji wa tatizo hilo la afya. Hii ni kwa kuwa njia ya sasa inahusisha daktari kuingiza kidole katika kuta za njia ya haja kubwa, jambo hili linaweza likawa la kihistoria kwa msaada wa teknolojia ya AI.
Wanasayansi nchini Korea Kusini wamefanikiwa kutengeneza kifaa cha upimaji wa tezi dume kwa kupima mkojo. Kipimo hicho kinaendeshwa na teknolojia ya kompyuta kwenye mfumo wa AI (Artificial Intelligence).
Wanasayansi hao wamesema ili kuweza kutengeneza kifaa hicho chenye uwezo wa kupata matokeo sahihi kwa takribani asilimia 100 umehusisha kuipa kompyuta uwezo wa kupima mamia vitu kwenye mkojo ili kuipa uwezo wa kuja na matokeo ambayo yanakuwa yana usahihi kwa kiwango kikubwa.
AI imewezaje kutumika?
AI ni mfumo wa akili bandia ya kompyuta inayokuwa na uwezo wa kuchambua data kwa urahisi na uharaka. Ili kuwezesha vifaa hivi kuwa na uwezo wa kupata matokeo yaliyosahihi tena ndani ya dakika ishirini tuu watafiti hao wameipa mashine data za kiafya za watu wenye matatizo ya tezi dume na data za kiafya za watu wasio na matatizo ya tezi dume, kwa kutumia data hizo kompyuta inapopima mkojo inafanya uchambuzi chembe zote za kibaiolojia zilizopo kwenye mkojo kwa kulinganisha data hizo zingine.
Ni kwa miaka mingi wanasayansi wamekuwa wakikuna vichwa na kufanya tafiti mbalimbali za kutafuta njia nyingine ya upimaji wa tezi dume.
No Comment! Be the first one.