Maswali yanaweza yakawa ni mengi sana juu ya simu yako ya zamani wakati ukiwa umepata simu mpya sio? .. wengi huwa wanafikiria kugawa na wengine kuuza simu hizo. Hakuna chaguo sahihi na chagua ambalo sio sahihi kwani itategemea na matakwa ya mmiliki wa kifaa hicho.
Lakini tuchukulie kwamba unataka kuuza simu janja yako ya zamani lakini cha msingi kujua hapa ni kwamba hutapata kiasi ambacho ni sawa sawa na ulichonunulia simu hiyo.. mfano simu janja ulinunua shilingi hamsini usitegemee baada ya kuitumia bado utaweza iuza kwa bei hiyo hiyo.
Cha msingi hapa ni kwamba, jitahidi kadri ya uwezo wako katika kutunza kifaa hicho, hii itasaidia simu janja hiyo ibaki katika hali nzuri ambayo itakuwezesha kuiuza kwa bei ambayo ina unafuu, tofauti kabisa na simu ikiwa imechoka!
Sawa Umeshakua Maamuzi Kwamba Unauza Simu janja Yako, Chukua Hatua Hizi Basi……
- Tambua/Jua Thamani Ya Simu Hiyo
Thamani ya simu hiyo katika hali yake unaweza kuijua kwa kufanya uchunguzi kidogo. Ulizia sehemu mbalimbali kwanba simu iliyotumika katika hali hiyo inaweza uzwa kwa kiasi gani. Njia ya haraka kabisa ni kuingia katika mtandao na kuanza kuulizia simu hiyo. Utapata ufumbuzi mwingi hii ni ikiwepo na bei ya kuuza simu janja hiyo.
Mitandao kama eBay, kupatana na mingine mingi itakusaidia sana katika kuhakikisha unapata bei ya simu janja husika, kulingana na hali ambayo kipo nayo.
2. Amua Namna Ya Kupokea Malipo
Je unataka kulipwa vipi? je simu hiyo utaiuza mtandaoni au biashara itafanyika ana kwa ana? ni mambo ya msingi sana ya kujiuliza kabla ya kuendelea na zoezi la kuuza simu hiyo. Ukishajua kuhusiana na yote vile vile kumbuka kuwa mnunuzi nae anaweza kagua simu hiyo na bado akaja na bei yake ambayo anapendezwa nayo kuuziwa (kulingana na hali ya simu hiyo).
Kabla ya hatua hii kumalizika vile vile ni muhimu sana kwa pande zote mbili kukubaliana vigezo na masharti kwenye biashara hiyo, vitu kama urejeshaji wa simu (mteja akishanunua) na mambo mengine yote ya muhimu inabidi yaongelewe na pande zote mbili.
3. ‘Back Up’ Na Kisha ‘Reset’ Simu
Kama katika simu hiyo kutakua na vitu vyako vya msingi kama vile namba za simu, picha n.k unaweza ukazihifadhi mtandao kwa njia kama hizi baada ya hapo zoezi linalofuata ni kufuta kila kitu katika simu hiyo. Hili lina fahamika kama ‘Reset’ ili kuirudisha katika hali yake ya mwanzo kabisa.
No Comment! Be the first one.