Uchumi duniani kote umetetereka kutoka na janga la virusi vya Corona ambavyo vimesababisha shughuli nyingi za kijamii, kisiasa, n.k kusimama ili kukabiliana na janga hilo lakini kwa namna moja au nyingine ni muhimu kutafuta mbaldala wa kupata riziki, sasa kuna Uber Connect na Uber Direct!
Hivi sasa hakuna dereva wa Uber duniani kote atakayekwambia kuwa biashara hiyo inamlipa bali ni hasara tuu au kupata kidogo kuliko vile ambavyo alikuwa akiingiza hapo mwanzo. Hata hivyo, tatizo la virusi vya COVID-19 vimeifanya kampuni ya Uber kwenye mataifa kama Marekani, Australia na Mexico kuanzisha huduma mbili za kipekee kabisa wakati huu ambao hakuna mzunguko mkubwa wa biashara.
Huduma hizo mpya ni Uber Connect na Uber Direct ambazo kila moja haziingiliani majukumu yake. Sasa, Uber Direct inatoa huduma kutoka duka la dawa, nyumba za kuhifadhia wanyama wadogo kwenda kwa mteja huku Uber Connect yenyewe ni kusafirisha mzigo kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Ni suala lisilopingika kwamba nchi zetu za Afrika zinahitaji mfumo huo wa usafirishaji wa bidhaa kutoka sehemu moja hadi nyingine hasa wakati huu ambapo madereva wengi wanashindwa kujipatia kipato ipasavyo kutokana na tatizo lililoikumba dunia. Je, wewe una mawazo gani?
Vyanzo: TechCrunch, The Verge