Moja ya kivinjari ambacho watumiaji wengi wa simu janja wanakitumia ni Google Chrome na ni wazi kuwa kutokana na ukuaji wa teknolojia uhalifu wa kwenye mtandao nao pia umeshika kasi jambo ambalo linafanya makampuni kuboresha ulinzi kwenye bidhaa za kidijiti wanazozimiliki.
Watu wengi ambao wanapenda kupata kile wanachokitafuta huwa wanperuzi tuu kwa kutumia kivinjari ambacho kipo tayari kwenye simu; kama ni rununu ya Android moja kwa moja Chrome inakuwepo ndani na iwapo unatumia iPhone, iPad basi kivinjari cha Safari kinahusika.
Katika hali ya kukabiliana na uhalifu unaohusisha mambo ya teknolojia hivi sasa kwenye kivinjari cha Chrome mhusika ataweza kupata taarifa iwapo mtu amejaribu kuweka nenosiri kwenye akaunti isimhusu ili kuweza kuingia ndani. Chrome inatoa taarifa kwa zile huduma zote ulizokubali kivinjari husika kiweze kukumbuka nywila.
Baada ya mhusika kupata taarifa kuwa akaunti yake (nenosiri) ya kwenye huduma fulani kuna mtu amejaribu kuitumia hapohapo atakuwa na uwezo wa kuangalia na kuweza kubadilisha nywila kwenye huduma husika. Katika kufanikisha hili Chrome inatuma taarifa kuhusu jaribio la kuingia kwenye akaunti kwenda Google katika muundo wa kuficha (encrypted) ambapo anayepokea taarifa (Google) anakuwa hajui jina maalum (username) na nywila ya mhusika.
Yanayokuja kwenye Chrome ya simu
Katika siku za usoni mtu ataweza kuangalia iwapo nenosiri la akaunti yake kenye huduma fulani imejaribiwa kutumiwa na mtu mwingine kupitia “Safety check” na iwapo kipengele cha “Safe browsing” kimeruhusiwa bila kusahau kuwa toleo la karibuni kabisa. Kwenye iOS watu wataweza kutumia kipengele cha barua pepe (jina maalum) na nywila kujijaza zenyewe kitendo hicho kitahitaji kuthibitishwa kwa alama ya kidole, sura kabla ya kufanyika.
HIvyo ndivyo ulinzi unavyozidi kuboreshwa ili kukabiliana na wale ambao wanapenda kuingia kwenye akaunti za watu jambo ambalo linahatarisha faragha ya mtu mtandaoni.
Vyanzo: Gadgets 360, GSMArena
No Comment! Be the first one.