Unapozungumzia suala zima la usalama wa vifaa vya kidijiti katika dunia ya leo ni wazi kwamba kampuni mbalimbali zinafanya juhudi sana kuhakikisha bidhaa zao zinakuwa salama. Sasa kivinjari cha Chrome kimeboreshwa zaidi kiusalama.
Kama ulikuwa hufahamu ni kwamba kinjari cha Chrome ambacho kinaweza kutumika kwenye rununu/kompyuta kimeazimisha miaka kumi (10) tangu kuanzishwa kwake na katika maadhimisho hayo wahusika wameamua kuongeza ulinzi wa kutumia alama ya kidole.
Uboreshwaji huo wa kivijari hicho umekwenda mbali zaidi na unaweza kutambua sura (bila kusahau pua, macho na mdomo), msimbomilia zote na sentensi iliyoandikwa kwa Kilatini katika mfumo wa picha kwenye mtandao.
“Msimbomilia” ni Kiswahili fasaha cha neno barcode kwa Kiingereza.
Google wametoa maboresho hayo kwa Android na iOS kwahiyo iwapo bado hujapokea masasisho cha kufanya ni kuhakikisha unatumia Chrome toleo la mwezi huu tarehe za karibuni kabisa.
Vyanzo: Engadget, The Verge